Loading...

Mnyama amaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kuu kwa vipigo viwili mfululizo.

NGUVU ya soda? Hilo ndilo swali unaloweza kujiuliza baada ya Simba SC kupoteza mchezo wa pili mfululizo leo kufuatia mwanzo mzuri katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Simba iliyoanza vyema Ligi Kuu na kucheza mechi 13 mfululizo bila kupoteza, ikishinda 11 na sare mbili – ilipoteza mechi ya kwanza Jumapili kwa kufungwa na African Lyon 1-0 Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.


Jana imepoteza mchezo wa pili kwa kufungwa 2-1 na wenyeji Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Katika mchezo wa jana, shujaa wa Prisons alikuwa ni mchezaji wa zamani Rhino Rangers ya Tabora, Victor Hangaya aliyefunga mabao yote mawili, baada ya Jamal Simba Mnyate kutangulia kuifungia Simba.



Kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog anaonekana hana raha baada ya Simba kupoteza mechi ya pili mfululizo Ligi Kuu leo.

Mnyate alifunga dakika ya 43 akimalizia kwa kichwa krosi nzuri ya winga Shizza Ramadhani Kichuya kutoka upande wa kushoto.

Simba ikaenda kupumzika inaongoza 1-0 na dakika mbili tu baada ya kuanza kipindi cha pili Hangaya akaisawazishia Prisons akimalizia krosi ya Salum Bosco kabla ya kufunga la pili dakika ya 64 akimalizia kwa kichwa mpira wa adhabu wa Mohammed Samatta.

Simba SC ilipambana kusaka bao la kusawazisha, lakini bahati mbaya wakaishia kukosa mabao ya wazi.

Nafasi nzuri zaidi alipoteza Kichuya dakika ya 83 baada ya kupiga shuti kali na mpira ukatoka nje pembeni sentimita chache na dakika ya 85 akapiga kona maridadi iliyokwenda nje kidogo ya lango.

Kwa matokeo hayo, Simba SC inamaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu na pointi zake 35 baada ya kucheza mechi 15, wakifuatiwa na mabingwa watetezi, Yanga.

Kikosi cha Prisons kilikuwa; Andrew Ntala, Benjamin Asukile, Salum Kimenya, Leonsi Mutalemwa, James Mwasote, Njinjai Kazungu, Jumanne Elfadhil, Lambarti Sabiyanka, Mohemmed Samatta, Victor Hangaya na Salum Bosco.

Simba SC; Vincent Agban, Hamadi Juma, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga, Method Mwanjali, Jonas Mkude/Mussa Ndusha dk82, Shizza Kichuya, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo, Mwinyi Kazimoto/Ibrahim Hajib dk69 na Jamal Mnyate.

ZeroDegree.
Mnyama amaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kuu kwa vipigo viwili mfululizo. Mnyama amaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kuu kwa vipigo viwili mfululizo. Reviewed by Zero Degree on 11/10/2016 10:12:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.