Loading...

TANZIA: RPC wa mkoa wa Singida afariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Peter Kakamba, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua maradhi ya tumbo, Jeshi la Polisi limethibitisha.

Akizungumza na wandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Mayala Towo amesema Kamanda Kakamba amefia hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Kaimu Kamanda Towo alithibitisha taarifa zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii mapema leo kuwa SACP Kakamba ameaga dunia, baada ya kukosa ushirikiano kutoka kitengo cha mawasiliano cha Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyokuwa inasambazwa kupitia mtandao wa WhatsApp mapema asubuhi, ilimnukuu Inspekta wa Jeshi la Polisi (IGP) Ernest Mangu akisema: “IGP anasikitika kutangaza kifo cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP Peter Kakamba kilichotokea usiku wa saa nne katika Hospitali ya Muhimbili DSM.

Kamanda Kakamba alikuwa amelazwa hospitalini hapo kwa maradhi ya tumbo alikuwa amefanyiwa operesheni hivi karibuni.”

Kwa mujibu wa Towo, mwili wa marehemu Kakamba utawasili Singida kwa ajili ya kuagwa kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao mkoani Rukwa kwa ajili ya maziko.

ZeroDegree.
TANZIA: RPC wa mkoa wa Singida afariki dunia. TANZIA: RPC wa mkoa wa Singida afariki dunia. Reviewed by Zero Degree on 11/30/2016 10:44:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.