Loading...

Wasichana wapelekwa mahakamani baada ya kuonekana wakipigana busu nchini Morocco.

Mahakama nchini Morocco.
Wasichana wawili waliopatikana wakipigana busu katika paa la nyumba wamewasilishwa mahakamani katika mji wa Marrakesh nchini Morocco wakishtakiwa na tabia za wapenzi wa jinsia moja ,mmoja wa mawakili wao waliambia AFP.

Wasichana hao wenye umri wa miaka 16 nad 17 mtawalia walishtakiwa kwa kushiriki tendo lililo kintume na maumbile yao.

Wawili hao walikamatwa mwezi uliopita baada ya kuripotiwa na familia zao.

Walipatikana wakikumbatiana na kupigana busu juu ya paa.

Wasichana hao wanakabiliwa na vifungo vya miezi sita hadi miaka mitatau jela.

Walikana yale yalioandikwa katika ripoti ya polisi kwamba walikuwa wakifanya vitendo vya wapenzi wa jinsia moja na kusema kuwa uhusiano wao ni wa kirafiki.

Source: BBC Swahili
ZeroDegree.
Wasichana wapelekwa mahakamani baada ya kuonekana wakipigana busu nchini Morocco. Wasichana wapelekwa mahakamani baada ya kuonekana wakipigana busu nchini Morocco. Reviewed by Zero Degree on 11/28/2016 06:14:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.