Loading...

Bei mpya za Petrol, Diesel na Mafuta ya Taa zinazoanza kutumika leo January 4, 2017.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini (EWURA) imetangaza bei mpya za Petrol, Diesel na mafuta ya Taa zinazoanza kutumika leo Jumatano huku bei ya mafuta ya Taa na Diesel ikiwa imeshuka kwa wastani wa shilingi 66 kwa lita.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Felix Ngamlagosi inaonesha kuwa kwa wastani kumekuwa na ongezeko dogo sana la bei ya mafuta ya Petroli ambayo kwa jiji la Dar es Salaam bado itauzwa kwa bei ile ile ilivyokuwa mwezi wa 12, 2016.

Hata hivyo, taarifa hiyo imetoa ruhusa kwa wauzaji wa jumla na rejareja wa mafuta nchini kuuza bidhaa hiyo kwa bei ndogo zaidi chini ya bei elekezi iliyotangazwa na mamlaka hiyo ikiwa ni njia ya kuongeza ushindani kati ya wauzaji wa nishati hiyo nchini.

ZeroDegree.
Bei mpya za Petrol, Diesel na Mafuta ya Taa zinazoanza kutumika leo January 4, 2017. Bei mpya za Petrol, Diesel na Mafuta ya Taa zinazoanza kutumika leo January 4, 2017. Reviewed by Zero Degree on 1/04/2017 12:13:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.