Loading...

Boniface Mkwasa atambulishwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga

MCHEZAJI na kocha wa zamani wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa leo ametambulishwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo, akichukua nafasi ya Baraka Deusdedit anayerejea kwenye Idara yake ya Fedha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga alisema kwamba Mkwasa anaanza majukumu yake rasmi Februari 1, mwaka huu.

Na Mkwasa anarejea Yanga ndani ya mwezi mmoja tangu aondolewe timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na nafasi yake kupewa Salum Mayanga.

Mkwasa aliifundisha Taifa Stars tangu Julai mwaka 2015 baada ya kurithi nafasi ya Mholanzi, Mart Nooij na katika kipindi chake aliiongoza timu hiyo katika mechi 13, ikishinda mbili, kufungwa sita na sare tano.
Boniface Mkwasa atambulishwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Boniface Mkwasa atambulishwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Reviewed by Zero Degree on 1/31/2017 12:21:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.