Loading...

Katiba ya Chama Cha Mapinduzi [CCM] yafanyiwa marekebisho

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Magufuli
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimefanya marekebisho ya katiba na kanuni za chama pamoja na jumuiya zake baada ya kufanya mabadiliko makubwa ikiwamo kupunguza idadi ya wajumbe wa Kamati na Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho.

Marekebisho hayo ambayo yatapitishwa rasmi katika mkutano maalumu utakaoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Rais John Magufuli utafanyika Machi 12, mwaka huu mkoani Dodoma, yametokana na uamuzi wa Halmashauri Kuu ya chama hicho, iliyofanyika Desemba mwaka jana jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo imesema mkutano huo pia utapokea taarifa ya ratiba ya uchaguzi mkuu wa chama hicho na jumuiya zake utakaofanyika nchi nzima baadaye mwaka huu.

“Mkutano mkuu huu pia utatanguliwa na mikutano ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Machi 10, na wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Machi 11, mwaka huu,” amesema.
Katiba ya Chama Cha Mapinduzi [CCM] yafanyiwa marekebisho Katiba ya Chama Cha Mapinduzi [CCM] yafanyiwa marekebisho Reviewed by Zero Degree on 3/02/2017 02:55:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.