Loading...

Rais Magufuli apiga simu Clouds TV na kuzungumza na Diamond Platnumz

Mwanamuziki Diamond Platnumz amepata nafasi ya kuzungumza na Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli kuhusu hali ya wasanii ilivyo nchini na kuomba serikali kuunga mkono juhudi zao ili kulisaidia taifa kuongeza pato na wasanii kupata faida kutokana na kazi wanazozifanya.

Diamond amezungumza na Rais Magufuli kupitia kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa katika kituo cha runinga cha Clouds Tv na kumwambia wamekuwa wakifanya jitihada lakini zaidi wanahitaji msaada wa serikali ili wapate kipato ambacho kinastahili kutokana na kazi wanayoifanya.

“Mkuu tunaomba utusaidie sana maana tunaamini wewe ni Rais ambaye unatetea wanyonge na kusaidia wanyonge na sisi vijana wako kwa unyonge wetu tunaomba utusaidie kwasababu utakuwa umesaidia familia nyingi, sababu tuna familia tuna watoto na watu wengi tunategemea mziki ili tujiajiri na kuliingia pato taifa,

“Nafikiri tuweke system nzuri ya kulipa kodi kama mimi ni mlipa kodi mzuri na wengine nimeweka mfumo wafate hivyohivyo nafikiri itasaidia sana kuliingizia pato taifa na sisi pia atleast kupata riziki na kujenga nchi yetu,” alisema Diamond.

Rais Magufuli alimjibu kwa kumpongeza kwa kazi nzuri ambayo wasanii wanaifanya ya kuitangaza Tanzania kimataifa, “Asante sana nimekusikia lakini pia nakupongeze na uzidi kuitangaza Tanzania katika muziki na hata wasanii wengine hata wale wanaoigiza nawapenda kama shilawadu na kadhalika.”

Lakini awali akizungumza na mtangazaji wa kipindi hicho Babbie Kabae alisema kuwa amepanga kukutana na wasanii ili kusikiliza changamoto zinazowakabili, “Maombi yake nimeyasikia nimepanga siku moja kukutana na hao wasanii ili tuone jinsi gani tunawasadia.”
Rais Magufuli apiga simu Clouds TV na kuzungumza na Diamond Platnumz Rais Magufuli apiga simu Clouds TV na kuzungumza na Diamond Platnumz Reviewed by Zero Degree on 3/14/2017 06:27:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.