Loading...

Rais Shein asema Serikali yake haitishiki na tishio la kukatiwa umeme, ..asema wako tayari kutumia vibatari

Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dr Shein, amesema hatishwi na vitisho vya TANESCO vya kuikatia umeme Zanzibar kwa sababu ya deni la Umeme kwani deni sio la leo, deni lina zaidi ya miaka 20.

Dkt. Shein ametoa msimamo huo katika mkutano wake na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa Zanzibar mara aliporejea kutoka Indonesia ambapo alikwenda kuhudhuria mkutano wa nchi zilizopakana na bahari ya Hindi akiwakilisha Rais John Magufuli ambapo amesema deni linalodaiwa serikali italipa na yeye kama rais hana taarifa yeyote ya Zanzibar kukatiwa umeme ingawa hatarajii kitendo hicho kufanyika.

“Tungoje basi uzimwe kama nyie muna wasiwasi, mimi najua hawezi kuuzima, kwa sababu deni hatujaanza kudaiwa leo sisi. Miaka 20 imepita tunadaiwa, kwahiyo mimi sitaki niseme sana leo kwenye hili na kama watazima basi, tutawasha vibatari vyetu, hatuna tatizo sisi. Lakini sidhani Tanzania iliyomakini kama inaweza kufanya vitu kama hivyo na sina uhakika kama magazeti yameandika vizuri,” alisema Dkt. Shein

Hatua hiyo imekuja baada ya TANESCO kutoa siku 14 kwa wadaiwa Sugu wa umeme kulipa vinginevyo watakaitwa umeme. Zanzibar inadaiwa deni la umeme zaidi ya Bil 121.
Rais Shein asema Serikali yake haitishiki na tishio la kukatiwa umeme, ..asema wako tayari kutumia vibatari Rais Shein asema Serikali yake haitishiki na tishio la kukatiwa umeme, ..asema wako tayari kutumia vibatari Reviewed by Zero Degree on 3/10/2017 12:34:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.