Loading...

Ujumbe wa Torres kwa kiungo wa Deportivo aliyemjeruhi kichwani hadi kumfanya apoteze fahamu

Baada ya kupata majeraha ya kichwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania, La Liga dhidi ya Deportivo La Coruna, na kupoteza fahamu, straika huyo wa Atletico Madrid alishazinduka na kunzungumza kuzungumza vizuri.

Katika pambano hilo lililomalizika kwa sare ya bao 1-1, Torres alilazimika kukimbizwa hospitali baada ya kugongana kichwani na kiungo mkabaji wa Atletico, Alex Bergantinos, hali iliyompelekea kupoteza fahamu.



Lakini baada ya matibabu ya haraka, staa huyo aliyewahi kuzichezea timu za Chelsea na Liverpool, alizinduka na kuzungumza na mashabiki wake pamoja na kumpa ujumbe, aliyemsababishia hali hiyo.

“Nawashukuru nyote mlioniombea hali yangu ni njema na nina matumaini nitarejea uwanjani hivi karibuni,” aliandika Torres kwenye mtandao wake wa Instagram.

Kuhusu Bergantinos aliyekwenda kumtembelea hospitali baada ya pambano kumalizika pale Estadio Riazor, alikutana kwanza na wahudumu kisha baadae kuonana na Torres ambaye alimpa ujumbe mzito uliomtia simanzi.

“Anaendelea vizuri na ana furaha sana. alisimuliwa tukio zima na amekuwa muelewa wa kuelewa kila kitu,” alisema Bergantinos.

“Aliniambia nitulie kwa sababu hivi ni vitu vya kawaida kwenye soka na si mara ya kwanza kutokeo. Nilichomfanyia mimi angeweza kufanyiwa na mwingine au yeye kumfanyia yotote, mchezo wa soka uko hivyo.

“Aliongea akiwa na tabasamu na anakumbuka mchezo wote ulivyokuwa kabla hajapata majeraha, ni jambo jema kuona amepona na atarudi tena uwanjani.”
Ujumbe wa Torres kwa kiungo wa Deportivo aliyemjeruhi kichwani hadi kumfanya apoteze fahamu Ujumbe wa Torres kwa kiungo wa Deportivo aliyemjeruhi kichwani hadi kumfanya apoteze fahamu Reviewed by Zero Degree on 3/05/2017 11:28:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.