Loading...

Aliyekuwa mshindi wa mbio za Olimpiki toka Kenya abainika kutumia dawa za kuongeza nguvu

Jemima Sumgong amebainika kutumia dawa za kusisimua misuli
Mwanariadha wa mbio za masafa marefu kutoka nchini Kenya, Jemima Sumgong aliyeshinda medali ya dhahabu katika mashindano ya mbio za marathoni olimpiki mjini Rio mwaka jana pamoja na mashindano ya mbio za London marathoni, amebainika kuwa ni miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kusisimua misuli.

Shirikisho la riadha duniani, IAAF limesema kuwa majibu waliyopata kutoka katika uchunguzi wa kina katika damu ya mwaariadha huyo umeonyesha kuwa anatumia dawa za kusisimua misuli ambazo zinamsaidia kukimbia kwa nguvu na kwa muda mrefu.

Jemima Sumgong
Mpaka sasa hakuna tamko lolote lililotolewa kutoka kwa mamlaka husika juu ya adhabu itakayotolewa baada ya majibu ya matokeo ya vipimo vya mwanariadha huyo.
Aliyekuwa mshindi wa mbio za Olimpiki toka Kenya abainika kutumia dawa za kuongeza nguvu Aliyekuwa mshindi wa mbio za Olimpiki toka Kenya abainika kutumia dawa za kuongeza nguvu Reviewed by Zero Degree on 4/07/2017 01:19:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.