Loading...

Ngome ilivyoisaidia Chelsea kunyakua Ubingwa wa Ligi Kuu

Kocha wa Chelsea, Antonio Conte ameisifu safu ya ulinzi ya klabu hiyo inayoongozwa na John Terry kwamba ndiyo imewapa ubingwa na matokeo mazuri msimu huu.


Chelsea iliibuka na ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Watford juzi ukiwa ni ushindi wa nane wa John Terry kwenye mechi ya Ligi Kuu kila timu hizo zilipokutana.

Conte alisema mchezaji huyo mwenye miaka 36 amekuwa msaada mkubwa kwenye kikosi hicho jambo lililofanikisha matokeo mazuri katika msimu huu.

“John natarajia kumuona akinyanyua kombe baada ya mchezo wetu dhdi ya Sunderland Jumapili wiki hii. Nafikiri wachezaji wenzake wanataka pia kumuona,” alisema Conte alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari” 

John alinisaidia sana katika msimu wangu wa kwanza ndani nan je ya uwanja. Amekuwa ni mchezaji ambaye amekuwa akiwapa moyo wacheaji wenzake kwenye msimu huu.

John alifanya uamuzi wa kucheza kila mechi na msimu huu alikuwa anapenda kuondoka Chelsea. Iwapo ataondoka jambo hilo litakuwa ni pigo kubwa kwetu.

Hata hivyo inatakiwa kuheshimu uamuzi wake

Kwa unapofika umri kama huu iwapo akili inakutuma kucheza unaweza kufanya hivyo .

Hata hivyo licha ya Terry kufunga bao lake jingine msimu huu, kocha Conte bado anaamini mchezaji huyo ataendelea kukisaidia kikosi hicho msimu ujao.
Ngome ilivyoisaidia Chelsea kunyakua Ubingwa wa Ligi Kuu Ngome ilivyoisaidia Chelsea kunyakua Ubingwa wa Ligi Kuu Reviewed by Zero Degree on 5/16/2017 06:56:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.