Loading...

Wawili wapandishwa kizimbani kwa kuisababishia TCRA hasara ya bilioni 2

Wakazi wa Zanzibar, Kalrav Patel(37) na Kamal Ashar (59) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka saba likiwemo la kusababisha hasara ya Sh 2 bilioni kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa leo amedai kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbroad Mashauri kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo 2015 kati ya Mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar.

Washtakiwa hao wanatetewa na Wakili John Mapinduzi wanadaiwa kuwa katika maeneo hayo ya Dar es Salaam na Zanzibar walikula njama ya kutaka kusafirisha vifaa vya mawasiliano bila kibali.

Ilidaiwa kuwa katika kipindi hicho 2015, washtakiwa hao walisafirisha vifaa vya mawasiliano kinyume na sheria za TCRA .

Kishenyi amedai kuwa mbali na mashtaka hayo washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka la kuingiza, kusimika nchini kifaa cha mawasiliano aina ya Voice Over internet protocol (Coop) na kukitumia bila ya kuthibishwa na TCRA.

Wawili wapandishwa kizimbani kwa kuisababishia TCRA hasara ya bilioni 2 Wawili wapandishwa kizimbani kwa kuisababishia TCRA hasara ya bilioni 2 Reviewed by Zero Degree on 5/09/2017 12:47:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.