Loading...

Mfalme wa Saudia amfuta kazi mrithi wake

Mfalme Salman wa Saudia amemfuta kazi mrithi wake
Mfalme Salman wa Saudia amebadilisha mkondo wa urithi na kumfanya mwanawe wa kiume Mohammed bin Salman kuwa mwanamfalme na kuwa wa kwanza kumrithi.

Mohammed Salman kushoto achukua nafasi ya Mohammed Nayef
Aliyekuwa mwanamfalme Mohammed bin Nayef amepokonywa taji lake na kufutwa kazi kama waziri wa maswala ya ndani.

Mohammed bin Salman mwenye umri wa miaka 31 ataendelea kuwa waziri wa ulinzi mbali na kuwa naibu waziri mkuu.

Mabadiliko hayo yalitangazwa katika misururu ya amri za kifalme.

Chombo cha habari cha Saudia kimesema kuwa mfalme ametaka raia wa taifa hilo kumtii mwanamfalme huyo mpya siku ya Jumatano.
Mfalme wa Saudia amfuta kazi mrithi wake Mfalme wa Saudia amfuta kazi mrithi wake Reviewed by Zero Degree on 6/21/2017 01:30:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.