Loading...

Serikali imetoa ajira kwa walimu 3,000

Naibu Waziri wa TAMISEMI Suleimani, Jafo Bungeni
Serikali imesema kuwa kwa mwaka 2017 imeweza kuajiri walimu elfu tatu na themanini wa masomo ya Sayansi na hisabati ambao wameshapangiwa kuripoti katika shule walizopangiwa nchi nzima.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa TAMISEMI, Suleimani Jafo Bungeni mjini Dodoma alipoulizwa swali na Jamali Kassim kwa niaba ya Issa Ally Makungu kwamba Serikali ilitoa mafunzo kwa walimu ambao walihitimu mwaka 2015 lakini walimu hao hawajaweza kuajiriwa Je, Serikali inampango gani wa kuajiri walimu hao.

Akijibu swali hilo, Jafo alisema kuwa Ajira hizo zimetolewa kwa walimu waliohitimu mafunzo mwaka 2015 na 2016, ambapo mpango wa Serikali ulikuwa ni kuajiri walimu elifu nne miamoja na 29, hatahivyo walimu elfu moja na 48 wa masomo ya Sayansi na hisabati hawakupatikana katika soko wakati wa uhakiki wa vyeti feki uliofanywa na wizara ya sayansi na teknolojia.

Hata hivyo Naibu waziri huyo ameongeza kwa kusema Serikali kupitia TAMISEMI imepanga kuajiri watumishi wa kada mbali mbali wakiwemo walimu katika mwaka wa fedha 2017 na 2018.
Serikali imetoa ajira kwa walimu 3,000 Serikali imetoa ajira kwa walimu 3,000 Reviewed by Zero Degree on 6/16/2017 08:20:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.