Loading...

Marekani kuziwekea wikwazo nchi za Urusi, Iran na Korea Kaskazini

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un anashutumiwa kwa kuibua silaha hatarishi za nyuklia kila kukicha
Baraza la wawakilishi la Marekani limepiga kura kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi, Iran na Korea Kaskazini.

Urusi inaadhibiwa kutokana na kudaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka jana wa Marekani huku Korea Kaskazini na Iran wao wakiadhibiwa kufuatia majaribio ya makombora.

Muswada huo unatarajiwa kupitia kwa baraza la seneti kabla ya kupelekwa kwa Rais Trump ili audhinishe na kuwa sheria kamili.

Akizungumza katika baraza hilo wawakilishi David Ciciline kutoka chama Democratic amesema hatua kamili zinahitajika kuiwajibisha Urusi.

Amesema hawawezi kuruhusu dola nyingine kuingilia uchaguzi wao japokuwa Rais wao anapinga kuihusisha Urusi na uchaguzi uliopita.

Naye Ted Poe kutoka chama cha Republican amesisitiza kuwa muswada unaihusisha Korea kaskazini pia.

Mwenyekiti wa kamati ya mahusiano ya kimataifa ya bunge la Urusi Duma , Leonid Slutsky amesema hatua hizo mpya zitazorotesha uhusiano baina ya Urusi na Marekani.
Marekani kuziwekea wikwazo nchi za Urusi, Iran na Korea Kaskazini Marekani kuziwekea wikwazo nchi za Urusi, Iran na Korea Kaskazini Reviewed by Zero Degree on 7/26/2017 08:12:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.