Loading...

Nape atabiri mshindi wa Urais Kenya


Mbunge wa Mtama, Nape Moses Nnauye amefunguka na kumtabiria ushindi mgombea Urais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na kusema kuwa atashinda uchaguzi huo ambao utafanyika Alhamisi Oktoba 26, 2017 na kusema Uhuru ndiye anayestahili kuongoza nchi hiyo.

Nape Nnauye amedai kuwa Uhuru Kenyatta anastahili kuwa Rais wa Kenya kwa sababu yeye ni mwana demokrasia wa kweli hivyo anaamini raia wa Kenya watampa kura nyingi za kutosha na kumpuuza mpinzani wake Raila Odinga.


"Unastahili kuwa Rais wa Kenya. Mwana demokrasia wa kweli. Naamini ndugu zangu wa Kenya watakuchagua kwa kishindo kesho na kumpuuza kibaraka" ameaandika Nape Nnauye kupitia mtandao wake wa twitter.

Nchi ya Kenya kesho inategemewa kufanya uchaguzi wa marudio wa nafasi ya urais kufuatia mahakama ya juu nchi humo kufuta matokeo ya urais.
Nape atabiri mshindi wa Urais Kenya Nape atabiri mshindi wa Urais Kenya Reviewed by Zero Degree on 10/25/2017 07:07:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.