Loading...

Niyonzima: “Kama binad­amu mwingine, siwezi kujisikia vizuri kukaa nje”


KIUNGO wa Simba, Mnya­rwanda, Haruna Niyonzima, amefunguka kuwa anahofia kupoteza kiwango chake kuto­kana na kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Niyonzima alipatwa na mata­tizo ya enka na hajacheza mechi yoyote tangu Novemba, mwaka jana, baada ya kuumia mazoezini na kumsababisha kukosa mechi kadhaa za ligi kuu. Yupo nje ya uwanja hadi hivi sasa.

Kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la Championi, Haruna Niyonzima alisema kuwa, anajisikia vibaya kuona anakaa nje kwa muda mrefu huku akikosa mechi za ligi, kwa kuwa mpira ndiyo kazi yake anayoitegemea kukaa nje kuta­muathiri.

“Kama binad­amu mwingine, siwezi kujisikia vizuri kukaa nje ya kazi yangu kwa muda mrefu, kuta­niathiri mimi, maisha yangu ni mpira, kama sichezi mpira, nitajisikia vibaya zaidi ya una­vyofikiria kwa kuwa sina kazi nyingine zaidi ya mpira ambao ninautegemea.

“Timu yangu inanihitaji niweze kuisaidia na mimi ninahi­taji kuitumikia nisaidie kitu fulani, siwezi ku­furahi nipo nje sichezi mpira, furaha pekee niliyo nayo kwa sasa ni kutokana na kuona timu yangu inafanya vizuri kwenye ligi, lakini kuhusu hali yangu sijisikii vizuri kwa kweli.

“Sijajua bado nitarejea lini uwanjani kwa sababu bado naendelea na matibabu, namuomba Mungu anisaidie,” alisema Niyonzima.

Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, amethibitisha kuwa klabu hiyo itampeleka kiungo huyo nje ya nchi kwa ajili ya matibabu, baada ya kukamilisha taratibu zote ndani ya wiki hii.
Niyonzima: “Kama binad­amu mwingine, siwezi kujisikia vizuri kukaa nje” Niyonzima: “Kama binad­amu mwingine, siwezi kujisikia vizuri kukaa nje” Reviewed by Zero Degree on 1/29/2018 02:30:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.