Loading...

NEC yatakiwa kuzingatia Sheria za Uchaguzi


Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa matokeo ya ripoti ya uangalizi wa uchaguzi mdogo wa marudio kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha uliofanyika Februari 17, mwaka huu.

Ripoti hiyo imetolewa leo Machi Mosi jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga ambapo pia kituo hicho kimetoa mapendekezo kadhaa kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamoja na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Henga amesema LHRC inaitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuratibu chaguzi mbalimbali kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zilizopo bila kufungamana na itikadi zozote za vyama vya siasa.

LHRC imeitaka NEC kutumia maafisa wake waliopata mafunzo stahiki katika zoezi la usimamizi pamoja na kutoa elimu ya mpiga kura ili kuwezesha wananchi kufahamu sheria na taratibu za uchaguzi. Pamoja na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuviwajibisha vyama vinavyokiuka sheria na taratibu wakati wa kampeni.
NEC yatakiwa kuzingatia Sheria za Uchaguzi NEC yatakiwa kuzingatia Sheria za Uchaguzi Reviewed by Zero Degree on 3/01/2018 07:33:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.