Loading...

Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine


Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya chai Tanzania (TBT) na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI).

Katika taarifa ilitolewa na Ofisi ya Kurugenzi Mawasiliano Ikulu leo Mei 23, 2018 imeeleza kuwa Mhandisi Steven Daudi Mlote, ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya chai Tanzania (TBT) na kuongeza kuwa Mhandisi Mlote anachukua nafasi iliyoachwa wazi na mtangulizi wake Mh. Anne Makinda ambae amemaliza muda wake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo imeongeza kwamba uteuzi wa Mhandisi Mlote ulianza Mei 21, 2018.

Sambamba na hayo Rais Dkt John Magufuli amemteua Dkt. Geofrey Mkamilo kuwa Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Tanzania (TARI), uteuzi wake umeanza Mei 22, 2018 na anachukua nafasi ya Dkt. Fidelis Angelo Myaka ambaye amestaafu.
Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine Reviewed by Zero Degree on 5/23/2018 04:35:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.