Msuva aweka wazi siri ya mafanikio yake
Msuva alifanikiwa kuifungia timu ya taifa, Taifa Stars bao la kwanza katika mchezo dhidi ya Cape Verde kwenye ushindi wa mabao 2-0, mechi iliyochezwa mwanzoni mwa wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Msuva amesema kuwa amekuwa akitumia muda mwingi katika kujiimarisha mazoezini, hivyo kumfanya awe fiti kila kukicha.
“Siri ya mafaniko kwangu ni kutokana na kutumia muda mwingi kujiimarisha mazoezini kwa kujituma na ndiyo maana nimeweza kuwa hivi nilivyo.
“Hata katika timu yangu ya Difaa nimekuwa nikifanikiwa kufunga kutokana na kujitambua na kujituma, naona kitu cha kawaida kwangu kufunga, kocha amekuwa akinitegemea katika kikosi cha kwanza,” alisema Masuva.
Msuva aweka wazi siri ya mafanikio yake
Reviewed by Zero Degree
on
10/19/2018 03:20:00 PM
Rating:
