Loading...

Messi 'hana mfano wala mpinzani' - Xavi


Aliyekuwa kiungo wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Hisapnia, Xavi amemusifia aliyekuwa mchezaji mwenzake Lionel Messi, akisema kwamba nyota huyo wa Barca anaweza kucheza soka kwa kiwango cha juu hata atakapofikisha miaka 40. Xavi alicheza na Messi kwa zaidi ya muongo mmoja katika klabu ya Barcelona na wawili hao pamoja na Andres Iniesta waliweza kushirikiana vizuri.

Kiungo huyo wa Al Sadd midfielder amemsifia Messi mara kadhaa na safari hii, ametamka kuwa Messi 'hana mfano'. Xavi alisema, “Wakati mwingine huwa nafikiri kwamba ataweza kucheza hata akifikisha miaka 38, 39 au 40. Ana mahitaji machache sana kuweza kufanikisha hilo. Ni kipi unachopoteza kadri umri wako unavyozidi kuongezeka? Kais yako? Vizuri, hata poteza kasi yake ya kufikiri. Messi hana mfano. Nafikiri kwamba ana uwezo wa kucheza popote pale anapotaka. Tayari anacheza hadi katikati ya uwanja na anapamudu, pia katika kuweka ukuta kwa sababu ana uwezo mkubwa wa kufikiri.”


Messi aliikosa mechi ya mwisho ya El Clasico na ya jana Copa Del Ray kwa sababu ya majeraha. Mechi ijayo ya Barcelona itakuwa dhidi ya Rayo Vallecano siku ya Jumapili.
Messi 'hana mfano wala mpinzani' - Xavi Messi 'hana mfano wala mpinzani' - Xavi Reviewed by Zero Degree on 11/01/2018 07:15:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.