CAF: Simba yakubali kichapo cha bao 2-0
Katika mchezo wa leo Simba walikuwa wamepoteana tangu kipindi cha kwanza ambapo kila mchezaji alicheza kama yupo Ligi Kuu Bara hali iliyowapa nafasi wapinzani wao JS Saoura kuwashambulia na kupata bao la kwanza dakika ya 18 ambalo lilidumu mpaka mapumziko.
Kipindi cha pili wachezaji wa Simba walionekana kujisahau tena na kuendelea kuutafuta mpira kama ni mchezo wa kirafiki huku wakishindwa kumiliki mpira.
Bao la pili la JS Saoura lilifungwa dakika ya 51 na kufanya matokeo kuwa 2-0 .
Matokeo hayo yanaipa wakati mgumu Simba kufuzu hatua ya robo fainali kutokana na milango kuwa migumu hasa kundi D ambalo kocha wa Simba Patrick Aussems alisema lipo wazi.
CAF: Simba yakubali kichapo cha bao 2-0
Reviewed by Zero Degree
on
3/09/2019 11:50:00 PM
Rating:
