Coman, Giroud waing'arisha Ufaransa ikishinda mabao 4-1
Ufaransa wakiwa nyumbani kwenye mchezo huo wa kufuzu Euro ilifanikiwa kuonyesha kiwango cha juu. Kiungo Kingsley Coman, alifanikiwa kufunga mabao mawili kwenye mchezo huo, huku mengine yakifungwa na Olivier Giroud na Jonathan Ikone.
Matokeo haya yanawafanya Ufaransa kujiweka kwenye sehemu nzuri ya kufuzu kwa fainali hizo za mwaka 2020.Pogba pamoja na Mbappe walionekana wakiwa jukwaani wakitazama mchezo huo huku mara kwa mara wakijadiliana baadhi ya mambo.
Hata hivyo, mechi hiyo ilichelewa kuanza kwa dakika saba baada ya makosa kufanyika badala ya kupigwa Wimbo wa Taifa wa Albania ukapigwa wa Andorra, ambapo wachezaji wa Albania waligoma kucheza hadi wimbo wao upigwe.
Coman, Giroud waing'arisha Ufaransa ikishinda mabao 4-1
Reviewed by Zero Degree
on
9/09/2019 10:55:00 AM
Rating:
