Kifusi chafukia watu 10 mgodini, mmoja afariki
Tukio hilo lilitokea juzi usiku wakati wakiendelea na shughuli za uchimbaji madini.
Imeelezwa kuwa baada ya wachimbaji kuingia ndani ya mashimo (mduara), ghafla kifusi kiliporomoka na kuwafukia watu 10 waliokuwamo ndani ya mgodi huo.
Aliyefariki dunia ni Ndaki Juma (45), mkazi wa Nyamikoma, Wilaya ya Busega mkoani Simiyu na majeruhi wametajwa kuwa ni Keo Werema, John Katwale, Mwita George, Masanja Charles, Abdallah Abdu, Bengwe Clement, Songa Charles, Emmanuel Mathias na Mangera Meki.
Akithibitisha kutokea tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro, alisema tayari majeruhi nane wameokolewa na kukimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa matibabu zaidi, huku mtu mmoja aliyefukiwa hajapatikana hadi sasa.
Kamanda Muliro alisema jeshi lake lilipokea taarifa za kutokea tukio hilo saa 7 usiku, ndipo askari kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Misungwi walifika haraka eneo la tukio.
“Jeshi la Polisi lilipokea taarifa za tukio la kuporomoka mgodi wa Shilalo, askari wetu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama tulifika mapema eneo la tukio na kufanikiwa kuwaokoa watu wanane, mmoja akiwa amefariki dunia na mwingine hajapatikana.
“Majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Wilaya Misungwi na juhudi za kumtafuta mwenzao zinaendelea kufanyika,” alisema Kamanda Muliro.
Imeelezwa kuwa baada ya wachimbaji kuingia ndani ya mashimo (mduara), ghafla kifusi kiliporomoka na kuwafukia watu 10 waliokuwamo ndani ya mgodi huo.
Aliyefariki dunia ni Ndaki Juma (45), mkazi wa Nyamikoma, Wilaya ya Busega mkoani Simiyu na majeruhi wametajwa kuwa ni Keo Werema, John Katwale, Mwita George, Masanja Charles, Abdallah Abdu, Bengwe Clement, Songa Charles, Emmanuel Mathias na Mangera Meki.
Akithibitisha kutokea tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro, alisema tayari majeruhi nane wameokolewa na kukimbizwa Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa matibabu zaidi, huku mtu mmoja aliyefukiwa hajapatikana hadi sasa.
Kamanda Muliro alisema jeshi lake lilipokea taarifa za kutokea tukio hilo saa 7 usiku, ndipo askari kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Misungwi walifika haraka eneo la tukio.
“Jeshi la Polisi lilipokea taarifa za tukio la kuporomoka mgodi wa Shilalo, askari wetu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama tulifika mapema eneo la tukio na kufanikiwa kuwaokoa watu wanane, mmoja akiwa amefariki dunia na mwingine hajapatikana.
“Majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Wilaya Misungwi na juhudi za kumtafuta mwenzao zinaendelea kufanyika,” alisema Kamanda Muliro.
Kifusi chafukia watu 10 mgodini, mmoja afariki
Reviewed by Zero Degree
on
9/11/2019 08:00:00 AM
Rating:
