Loading...

Wafungwa Afrika Kusini wapiga kura


Wafungwa katika Gereza la Usalama wa Juu la Pollsmoor walipiga kura asubuhi ya Jumatano (Mei 29) katika uchaguzi mkuu wa Afrika Kusini.

Walinzi waliwaongoza wafungwa nje kwa makundi yaliyodhibitiwa ili kufanya usajili wao wa kupiga kura, na kushiriki katika uchaguzi.

Waafrika Kusini wanapiga kura Jumatano katika uchaguzi wenye ushindani mkubwa zaidi tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi, huku kura za maoni zikionyesha kwamba chama cha African National Congress (ANC) kinaweza kupoteza wingi wake bungeni baada ya miaka 30 madarakani.

ANC bado iko njiani kushinda sehemu kubwa ya kura, ikimaanisha kwamba kiongozi wake Rais Cyril Ramaphosa anaweza kubaki madarakani, isipokuwa atakabiliana na changamoto ya ndani ikiwa utendaji wa chama utakuwa mbaya zaidi kuliko inavyotarajiwa.

Foleni zilishuhudiwa katika miji mikuu ya Johannesburg, Cape Town na Durban wakati upigaji kura ulianza asubuhi na mistari pia ilionekana kwenye vitongoji vya miji na katika maeneo ya vijijini.

Zaidi ya Waafrika Kusini milioni 27 wamesajiliwa kupiga kura katika vituo vya kupigia kura zaidi ya 23,000 vilivyoko katika shule, vituo vya michezo na hata kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti huko Pretoria.

Upigaji kura utaendelea hadi saa 3 usiku.

Chanzo: Voa
Wafungwa Afrika Kusini wapiga kura Wafungwa Afrika Kusini wapiga kura Reviewed by Zero Degree on 5/30/2024 07:20:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.