ATCL yasitisha safari za Afrika Kusini
Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa ATCL Ladislaus Matindi, na kuagiza mawakala wote kurejesha nauli za abiria, waliokuwa wamekwishakata tiketi kwa ajili ya safari na kwamba safari hizo zimesimamishwa hadi taarifa kamili itakapotolewa tena.
Ikumbukwe kuwa hapo awali, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, alitoa tamko rasmi la kusitisha safari za ndege hizo kufuatia vuguvugu la machafuko lililokuwa likiendelea Afrika Kusini, kati ya wazawa na raia wa mataifa mengine.
Mnamo Agosti 23, 2019,ndege ya ATCL aina ya Bombadier Q220 - 300, ilishikiliwa nchini humo kwa amri ya mahakama ya Guateng nchini humo, ambapo baadaye iliachiwa huru baada ya mawakili wa Serikali kuishinda kesi dhidi ya mkulima.
Ikumbukwe kuwa hapo awali, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, alitoa tamko rasmi la kusitisha safari za ndege hizo kufuatia vuguvugu la machafuko lililokuwa likiendelea Afrika Kusini, kati ya wazawa na raia wa mataifa mengine.
Mnamo Agosti 23, 2019,ndege ya ATCL aina ya Bombadier Q220 - 300, ilishikiliwa nchini humo kwa amri ya mahakama ya Guateng nchini humo, ambapo baadaye iliachiwa huru baada ya mawakili wa Serikali kuishinda kesi dhidi ya mkulima.
ATCL yasitisha safari za Afrika Kusini
Reviewed by Zero Degree
on
10/06/2019 03:35:00 PM
Rating: