Loading...

Jeshi lakomboa 300 kutoka kwa Boko Haram Nigeria.


Rais Buhari aliwapa wakuu wa jeshi miezi mitatu kuanzia Agosti 14 waangamize Boko Haram.

Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limefanikiwa kuwakomboa watu 338 kutoka kwa wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram.

Wapiganaji 30 waliuawa kwenye operesheni hiyo kwenye ngome moja ya kundi hilo katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo mnamo Jumanne.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi Kanali Sanni Kukasheka Usman, wanajeshi walishambulia kambi za wapiganaji hao kwenye msimu wa Sambisa na kukomboa watoto karibu 200, wanawake mia moja na wanaume wanane.

Mwandishi wa BBC aliye Abuja Chris Ewokor anasema kufikia sasa hakujatolewa maelezo zaidi kuhusu watu waliokombolewa.

Operesheni hiyo ni moja ya operesheni kubwa zaidi kufanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya wanamgambo hao.

Buhari ameahidi kuangamiza kundi la Boko Haram

Jeshi linaonekana kujikakamua kutimiza makataa ya miezi mitatu ambayo walipewa na Rais Muhammadu Buhari kuwashinda Boko Haram, ingawa muda unayoyoma.
Wanamgambo hao wamekuwa wakitekeleza mashambulio ya kujitoa mhanga na kuua watu wengi kaskazini mashariki mwa taifa hilo, wengi wao waumini wa dini ya Kiislamu misikitini.


Credits: BBC
ZeroDegree.
Jeshi lakomboa 300 kutoka kwa Boko Haram Nigeria. Jeshi lakomboa 300 kutoka kwa Boko Haram Nigeria. Reviewed by Zero Degree on 10/28/2015 05:43:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.