Loading...

Matokeo ya kidato cha pili hadharani, 89% wasonga mbele [ Kuyaona fuata kiunganishi hiki ].


Dk Charles Msonde

Dar es Salaam. Jumla ya wanafunzi 324,068 wa kidato cha pili sawa na asilimia 89.12 ya wanafunzi 363, 666 waliofanya mitihani ya upimaji mwaka jana wamefaulu kuendelea na masomo ya kidato cha tatu. (
BOFYA HAPA KUYAONA MATOKEO HAYO )

Akitangaza matokeo ya mitihani hiyo iliyofanyika nchi nzima kuanzia Novemba, 16 hadi 27, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani, Dk Charles Msonde amesema jijini Dar es Salaam leo kuwa jumla ya watahiniwa 164, 547 sawa na asilimia 89.00 ya watahiniwa wote wa kike waliofanya mitihani hiyo wamefaulu.

Amesema watahiniwa 159, 521 sawa na asilimia 89.24 ya watahiniwa wote wa kiume waliofanya mitihani hiyo nao wamefaulu huku wanafunzi 39, 567 sawa na asilimia 10. 88 wameshindwa kukidhi viwango vya kuwaruhusu kuendelea na kidato cha tatu.

Akifafanua kuhusu matokeo hayo, Dk Msonde amesema ufaulu umeshuka kwa masomo ya Uraia, Historia, Jiografia, Kiingereza, Fizikia, Biolojia, Hisabati na ‘Book Keeping’ ikilinganishwa na mwaka 2014.

Amesema ufaulu umepanda kidogo katika masomo ya Kiswahili, ‘Commerce’ na Kemia ikilinganishwa na ufaulu wa masomo hayo mwaka 2014.

Ameitaja mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Mbeya na Iringa kuwa ndiyo iliyotoa shule kumi bora huku shule kumi zilizofanya vibaya zikitoka mikoa ya Tanga Mtwara, Lindi na Dar es Salaam.

Katibu huyo amesema jumla ya wanafunzi 396, 770 waliandikishwa kwa ajili ya mitihani hiyo ya upimaji ambapo 33, 104 sawa na alimia 8.3 hawakufanya mitihani hiyo nchi nzima kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za utoro na maradhi.








Source: Mwananchi
Matokeo ya kidato cha pili hadharani, 89% wasonga mbele [ Kuyaona fuata kiunganishi hiki ]. Matokeo ya kidato cha pili hadharani, 89% wasonga mbele [ Kuyaona fuata kiunganishi hiki ]. Reviewed by Zero Degree on 1/15/2016 03:48:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.