Loading...

Mikataba ya Jeshi la Polisi kupitiwa upya.


BAADA ya Rais John Magufuli kuizungumzia mikataba ya ujenzi ya Jeshi la Polisi iliyoingia na wawekezaji, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ameitisha mikataba yote ya jeshi hilo.

Jeshi la Polisi nchini limetakiwa kuwasilisha mikataba ya miradi ya ujenzi wa nyumba za kuishi askari eneo la Kunduchi, Mikocheni pamoja na Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar es Salaam pamoja na ule wa majengo mbalimbali ya mwekezaji ambaye Jeshi la Polisi limeingia mkataba naye.

Agizo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira ikiwa ni miezi miwili tu tangu Rais Magufuli kuzungumzia mikataba hiyo na kuitilia shaka wakati akifungua kikao kazi cha makamanda wa Polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa mikoa na vikosi mjini Dodoma.

Meja Jenerali Rwegasira alisema mradi huo ni mkubwa na wa muda mrefu na hivyo ameliagiza jeshi hilo kuuwasilisha mkataba huo, ambao utekelezaji wake unaendelea ili aufahamu vizuri mkataba huo, unaolihusisha Jeshi la Polisi na Mwekezaji wa Kampuni ya Mara World Tanzania Limited.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo jana kwa vyombo vya habari, Katibu Mkuu huyo ametoa agizo hilo muda mfupi baada ya kukagua miradi hiyo katika maeneo ya Kunduchi na Mikocheni, ambako zinajengwa nyumba za kuishi askari wa Jeshi la Polisi na kwamba ujenzi wake bado unaendelea.

Source: Mtembezi
ZeroDegree.
Mikataba ya Jeshi la Polisi kupitiwa upya. Mikataba ya Jeshi la Polisi kupitiwa upya. Reviewed by Zero Degree on 6/06/2016 10:31:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.