Loading...

Tundu Lissu hali tete Kisutu, Mahakama yatupilia mbali ombi lake la kufutiwa mashitaka.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) ya kufutiwa mashitaka ya uchochezi yanayomkabili na wenzake watatu.

Tundu Lissu na wenzake kupitia kwa wanasheria wao waliwasilisha maombi yao katika mahakama hiyo ya kutaka mahakama kufuta mashtaka hayo kwa madai kuwa hati ya mashtaka imekosewa kwani haielezi vya kutosha kuhusu makosa wanayotuhumiwa kuyatenda.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilieza jana kuwa baada ya kupitia hoja za pande zote mbili (mshataki ambaye ni Jamhuri na mshtakiwa ambaye ni Tundu Lissu na wenzake) walijiridhisha kuwa hati hiyo haina makosa.

Watuhumiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kuchapisha habari ya uchochezi kwenye gazeti yenye kichwa cha habari kilichosomeka “Machafuko Zanzibar”. Habari hii ilichapishwa kati ya Januari 12-14 mwaka huuna inadaiwa ililenga kuwatisha wananchi wa Zanzibar wasijitokeze kwenye uchaguzi wa marudio Machi 20 mwaka huu.

Pamoja na na Tundu Lissu, washtakiwa wengine ni pamoja na mwandishi wa gazeti la Mawio, Jabir Idrissa, Mhariri wa gazeti hilo, Simon Mkina na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob.


Source: Swahili Times.
ZeroDegree.
Tundu Lissu hali tete Kisutu, Mahakama yatupilia mbali ombi lake la kufutiwa mashitaka. Tundu Lissu hali tete Kisutu, Mahakama yatupilia mbali ombi lake la kufutiwa mashitaka. Reviewed by Zero Degree on 7/17/2016 11:03:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.