Loading...

VIDEO: Barcelona walivyomdhalilisha kocha wao wa zamani, Pep Guardiola kwa kichapo cha bao 4 - 0.

Michuano ya klabu bingwa ulaya imeendelea kwa michezo nane kupigwa ambapo Arsenal waliiadhibu Ludogorets Razgrad ya Bulgaria 6-0, wakati Mesut Ozil akipata hat trick.

Messi amefunga magoli 10 katika michezo nane ya mwisho ya ligi ya mabingwa Ulaya.
Barcelona nayo wakiwa nyumbani walimdhalilisha kocha wao wa zamani Pep Guardiola kwa kumpa kichapo cha 4-0, Messi nae akipiga hat-trick, ambapo katika mchezo huo ilishuhudiwa mlinzi wa Man city Claudio Bravo akilambwa kadi nyekundu huku pia mlinzi wa Barcelona aliyeingia akitokea benchi Jeremy Mathieu naye akizawadiwa kadi nyekundu.

Bravo atakosa mchezo wa maruduiano Novemba 1.
Makosa ya wazi ya mlinzi wa Celtic Kolo Toure yakaipa Borussia Monchengladbach ushindi wa mabao 2-0 wakiwa ugenini, magoli yakifungwa na Lars Stindl pamoja na Andre Hahn.

Wachezaji wa Arsenal wakifurahia ushindi mnono.

Matokeo ya michezo mingine iliyochezwa jana.
  • Bayern Munich 4-1 PSV Eindhoven
  • Paris Saint-Germain 3-0 Basel
  • Dynamo Kiev 0-2 Benfica
  • Napoli 2-3 Besiktas
  • FC Rostov 0-1 Atlético Madrid
  • Arsenal 6-0 Ludogorets
  • Celtic 0-1 B. Monchengladbach

ZeroDegree.
VIDEO: Barcelona walivyomdhalilisha kocha wao wa zamani, Pep Guardiola kwa kichapo cha bao 4 - 0. VIDEO: Barcelona walivyomdhalilisha kocha wao wa zamani, Pep Guardiola kwa kichapo cha bao 4 - 0. Reviewed by Zero Degree on 10/20/2016 09:49:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.