Loading...

Bale ameshinda tena tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Wales.

Gareth Bale.
Winga wa timu ya taifa ya Wales ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Wales kwa mara ya nne mfululizo.

Bale mwenye umri wa miaka 27 kwa ujumla ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa nchi yake kwa mara sita.

Kiungo wa Stoke City Joe Allen ametwaa tuzo mbili tuzo ya wachezaji na tuzo ya washabiki, huku mchezaji wa timu ya Exeter City, Ethan Ampadu mwenye umri wa miaka 16 akitwaa tuzo ya chipukizi bora.

Ethan Ampadu mchezaji bora chipukizi.
Wachezaji wengine waliopata tuzo hizo ni kiungo Aaron Ramsey aliyepata tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya ulaya ya mwaka 2016.

Mshambuliaji Robson-Kanu akipata tuzo ya goli bora la michuano ya ulaya ya mwaka 2016, goli lililompa tuzo ni la mchezo wa robo fainali dhidi ya Ubelgiji.

Natasha Harding,amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka kwa upande wa Wanawake.

ZeroDegree.
Bale ameshinda tena tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Wales. Bale ameshinda tena tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Wales. Reviewed by Zero Degree on 11/09/2016 06:02:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.