Loading...

Gharama za viingilio katika mechi za Ligi Kuu ya Uingereza imeshuka.

GHARAMA ya kuhudhuria mechi ya soka ya Ligi Kuu ya England imeshuka katika msimu wa kwanza wa rekodi ya mkataba wa haki ya TV wa pauni bilioni 8. Uchunguzi huo wa aina yake umefanywa Ulaya, ambapo umeangalia viingilio vya klabu 223.

Kwa mujibu wa taarifa hizo karibu zaidi ya mbili ya tatu ya tiketi zote Ulaya ama zimepungua au zimebaki pale pale katika msimu wa mwaka 2016-17.

Hata hivyo, tiketi za kushuhudia mchezo wa ugenini katika mechi za Ligi Daraja la Kwanza sasa zinaonekana ziko bei juu kuliko zile za mechi za Ligi Kuu ya England.

Hii ni kwa sababu klabu kubwa zimepunguza viingilio vyake hadi pauni 30 kwa mashabiki wanaokuja kushuhudia mechi ugenini ili kuona pambano la Ligi Kuu. Malcolm Clarke, mwenyekiti wa Shirikisho la mashabiki wa soka alisema:

"Katika mkataba wao wa sasa wa pauni bilioni 8.3, Ligi Kuu imeweza kumuachia shabiki mmoja kuingia bure katika kila mchezo nab ado wana baki na fedha nyingi kama walivyokuwa nazo katika mkataba wa awali. Ligi Kuu ilieleza katika taarifa yake:

"Klabu zimekuwa zikiwasikiliza mashabiki wao na kuhakikisha soka la Ligi Kuu linaendelea kuwa bora siku hadi siku.”

Uchunguzi huo pia umebaini kuwa utengenezaji wa jezi na kuziuza kumeongeza mapato ya klabu kwa nusu ya klabu kubwa mwaka hadi mwaka.

Kwa mara ya kwanza, tuliziomba klabu asilimia ya kiasi fulani cha fedha za tiketi kutoka katika klabu za wanaume wakubwa, huku Southampton inabainisha kuwa moja kati ya mashabiki watano wenye tiketi za msimu ni wanawake wakati Liverpool wenyewe ni asimia 11.

Wastani wa gharama ya chini kwa mchezo wa nyumbani wa watu wazima kwa tieti ya mechi ya siku katika Ligi Kuu imeshuka hadi asilimia 6 kwa mwaka hadi mwaka (kutoka pauni 30.95 hadi pauni 29.05) Tiketi ya mechi ya ugenini imeshuka kutoka asilimi 37 (kutoka pauni 46 hadi kufikia pauni 29.44).

Wastani wa gharama ya juu kwa tiketi ya mchezo waLigi Daraja la Kwanza kwa sasa ziko juu zaidi ya zile za Ligi Kuu (pauni 31.57). Katika Ligi Kuu ya Scotland, kiingilio cha chini kwa mechi ya siku kimepanda kwa asilimi 1, ikiwemo kile cha timu iliyopanda daraja ya Rangers, na kuifanya kuwa pauni 20.58.

Lakini pamoja na kupanda lakini bado ni rahisi zaidi ya kiingilio cha Ligi Daraja la Kwanza ya Uingereza (pauni 22.11) Bei imepanda kwa asilimia 14 katika Ligi Kuu, wakati asilimia 34 ni rahisi zaidi ya mwaka uliopita na asilimi 53 imebaki pale pale haijapada wala kushuka.

Klabu tatu za Burnley, Middlesbrough na Leicester – ziliongeza bei zao nafuu za tiketi za mechi za siku lakini Hull City, Liverpool na Manchester City zilipunguza viingilio vyo, Wastani wa tiketi ya bei nafuu zaidi ya Ligi Kuu kwa msimu ni asilimia 480 ikiwa ni gharama ya chini zaidi ya ule wa mwaka 2013, wakati ule ilipokuwa pauni 489 Uchunguzi wa mwaka huu, uliozihusisha klabu 223 katika ligi 23 England, Scotland, Wales, Ireland na kwa Ulaya kwa ujumla.

Klabu zinavyotoza fedha Arsenal ndio klabu inayochaji kiasi kikubwa cha fedha kwa tiketi ya mechi ya siku wakitoza kiasi cha pauni 97,lakini bei hii haijapanda tangu mwaka 2014 Hull City na Liverpool ndio wenye gharama ndogo zaidi wanazotoza kwa mechi za siku za Ligi Kuu ya England, ambapo hutoza kiasi cha pauni 9.

Tiketi tatu ghali zaidi za msimu zote zinatokea jijini London, ambazo ni mechi ya Arsenal (pauni 2,013), Spurs (pauni 1,895) na Chelsea (pauni 1,250), lakini hizo zote hazikupanda kutoka mwaka 2015.

Pauni 252 za Hull City ndio kiingilio rahisi zaidi katika Ligi Kuu. Jezi zina gharama zaidi Asilimia 31 ya klabu zinazoshiriki Ligi Kuu nne za Uingereza ziliongeza bei yake ya jezi za watoto, huku Manchester United iichaji ghali zaidi (dola 50),.

Manchester United na Manchester City wanatoza pauni 60 kwa jezi za wakubwa, wakati Bournemouth na Burnley wanachaji kiasi cha chini katika Ligi Kuu-pauni 40.

Katika Ligi Kuu ya Scotland, Celtic inatoza kiasi cha pauni 53 kwa watu wazima, wakati Inverness Caledonian wanatoza kiasi cha pauni 35 kikiwa ni kidogo.

ZeroDegree.
Gharama za viingilio katika mechi za Ligi Kuu ya Uingereza imeshuka. Gharama za viingilio katika mechi za Ligi Kuu ya Uingereza imeshuka. Reviewed by Zero Degree on 11/19/2016 11:25:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.