Loading...

Hawa ndio walioongeza mikataba yao na Klabu ya Arsenal

Laurent Koscielny

Wachezaji wa Arsenal Olivier Giroud, Laurent Koscielny na Francis Coquelin wameongeza kandarasi zao na klabu hiyo.

Arsenal haijatangaza kuhusu kiwango cha kandarasi hizo ,lakini Koscielny amesema katika mtandao wa Twitter kwamba ataongeza kandarasi yake hadi mwaka 2020.

''Tunafurahi kwamba wachezaji watatu muhimu wameamua kusalia nasi kwa kipindi cha muda mrefu'', Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amenukuliwa akisema.

Mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud na bao lake la nge dhidi ya Crystal palace
Wachezaji hao wa Ufaransa wamekuwa wakishiriki kila mechi huku Giroud akiweka kandarasi hiyo baada ya kufunga mabao manne katika mechi nne likiwemo bao lake la 'nge' dhidi ya Crystal palace.

''Francis ameimarika pakubwa katika kipindi cha miaka michache iliopita kwa sababu ana maono kila siku'', alisema Wenger.

Francis Coquelin
''Olivier ana uzoefu katika mechi kubwa na ameimarika zaidi tangu ujio wake hapa. Koscielny ni kiungo muhimu wa kikosi chetu na ninaamini ni mmojawapo wa mabeki wazuri duniani''.

ZeroDegree.
Hawa ndio walioongeza mikataba yao na Klabu ya Arsenal Hawa ndio walioongeza mikataba yao na Klabu ya Arsenal Reviewed by Zero Degree on 1/12/2017 08:10:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.