Loading...

PSG wakaimilisha usajili wa nyota wa kimataifa toka taifa la Ujerumani, Julian Draxler.

Julian Draxler amekamilisha taratibu zote za uhamisho wake kuelekea klabu ya Paris Saint-Germain kutoka Wolfsburg.

Mipango ya uhamisho kwa nyota huyo wa kimataifa raia wa Ujerumani, mwenye umri wa miaka 23, ilianza wakati wa Krismasi lakini pande zote mbili zilikua bado hazijafikia makubaliano, jana Jumanne kndipo PSG walithibitisha kukamilisha uhamisho wa nyota huyo ikiaminika kuwa ada yake ya uhamisho ilikuwa ni dola za kimarekani milioni 43.5.

Hiki ndicho alichosema Draxler, mshindi wa Kombe la Dunia akiwa Ujerumani mwaka 2014 ambaye alikua na jukumu kubwa katika kufanikisha ushindi huo kwa taifa lake na vile vile alikuwa na nafasi kubwa wakati wa EURO mwaka 2016, alisema haya kuhusu kujiunga na Klabu ya PSG mabingwa watetezi
 kombe la ligue 1 nchini Ufaransa.


"Nitafanya kila kitu ili kusaidia PSG kushinda vikombe vimpya na kuendelea kukua katika soka kimataifa," Draxler alisema. "Mimi nina kwenda kugundua nchi na ligi mpya, na nina jisikia faraja sana kufikia hatua hii mpya ya kusajiliwa katika klabu ambayo imekuwa ya kuigwa katika ligi ya Ulaya na inmesajili wachezaji wengi wakubwa katika miaka ya hivi karibuni."

Pamoja na Arsenal kuonyesha nia ya kumsajili Draxler kwa miaka mingi, ni ajabu 
kidogo ameamua kwenda kujiunga na klabu ya Ligue 1 wakati kwa kawaida Ligi ya Uingereza (EPL) au La Liga ingekuwa chaguo zuri kwake kwa kujipima uwezo. 

Lakini binafsi yeye alisema kwamba, hilo si swala la kushangaza kwani yeye kaacha na Wolfsburg ambayo kwa sasa wako katika hali ngumu wapigana mwishoni mwa msimamo wa ligi ya Bundesliga.

PSG wamekuwa na wkati mzuri kiasi katika nusu ya kwanza ya kampeni ya kutafuta taji la msimu wa 2016-17 chini ya kocha mpya Unai Emery wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo nyuma ya Nice ambao ndio viongozi kwa pointi tano.

Kuwasili kwa Draxler mwenye kasi na ujanja mwingi, bila shaka kutaongeza kasi ya Angel di Maria na nguvu ya Edison Cavani wakati PSG ikitazamia kushinda taji la mara ya tano mfululizo katika Ligi hiyo ya Kifaransa na angalau kufanya vizuri walau hata kufika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa. 

Lakini mwishoni itakuwa ngumu kwa PSG ambao wanakutana na Barcelona katika Duru ya 16 bora, lakini uwezo wa kuongeza mchezaji mwwnyw ubora kama Draxler inatilia mkazo kuona ni kiasi gani PSG wana uwezo mkubwa wa kifedha PSG.

ZeroDegree.
PSG wakaimilisha usajili wa nyota wa kimataifa toka taifa la Ujerumani, Julian Draxler. PSG wakaimilisha usajili wa nyota wa kimataifa toka taifa la Ujerumani, Julian Draxler. Reviewed by Zero Degree on 1/03/2017 06:28:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.