Loading...

Mohamed Habibu atimuliwa kutoka Chama Cha Wananchi [CUF]

Chama cha Wananchi (CUF) kimemtimua uanachama Mohamed Habibu Mnyaa, huku mwenyewe akidai bado ni mwanachama halali.

Mnyaa amefukuzwa na mkutano mkuu wa tawi la Chanjaani, Jimbo la Mkoani kisiwani Pemba, uliohudhuriwa na wajumbe 112 kati ya 113.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa tawi la Chanjaani, Kombo Mohamed Maalim, ilisema Mnyaa alifukuzwa kutokana na kukiuka katiba ya chama hicho Ibara ya 12 (6)(7)(16).

Alisema miongoni mwa mambo aliyofanya ni kuwa na mwenendo usiofaa wa kuwagawa wanachama, kueneza taarifa za upotoshaji dhidi ya viongozi na chama, kufanya vitendo vya hujuma za kutaka kukidhoofisha chama, kudharau na kushindwa kuhudhuria na kutoa ushirikiano kwa tawi lake kila alipotakiwa kufanya hivyo.

Akizungumzia hatua hiyo, Mnyaa ambaye amewahi kuwa mbunge wa Mkanyageni kwa vipindi viwili mwaka 2005-2015 alisema hukumu ya kufukuzwa kwake imechukuliwa katika tawi ambalo siyo lake, kwa kuwa alishalihama tangu mwaka jana.

Source: Mwananchi
Mohamed Habibu atimuliwa kutoka Chama Cha Wananchi [CUF] Mohamed Habibu atimuliwa kutoka Chama Cha Wananchi [CUF] Reviewed by Zero Degree on 2/08/2017 12:17:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.