Loading...

Fainali ya ligi ya Europa kuchezwa leo kati ya Ajax na Manchester United

Mchezo huu wa fainali utachezwa katika dimba la Friends mjini Stockholm, kuanzia saa nne kasoro robo kwa saa za Afrika mashariki na mwamuzi wa mchezo huo atakua Damir Skomina raia wa Slovenia.

Mchezo huu ni muhimu zaidi kwa Manchester United ambao wamemaliza ligi katika nafasi ya sita katika ligi ya England, hivyo kama watashinda licha ya kutwaa kombe watapata tiketi ya kucheza michuano ya klabu bingwa ulaya msimu ujao.

Ajax tayari wana nafasi ya kucheza klabu bingwa ulaya msimu ujao kwa kuwa wamemaliza ligi ya kwao nchini Uholanzi wakiwa katika nafasi ya pili.
Fainali ya ligi ya Europa kuchezwa leo kati ya Ajax na Manchester United Fainali ya ligi ya Europa kuchezwa leo kati ya Ajax na Manchester United Reviewed by Zero Degree on 5/24/2017 10:12:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.