Loading...

Nape, Tundu Lissu, na Zitto Kabwe wafunguka kuhusiana na ripoti ya mchanga

Baadhi ya wabunge wameibua hoja tofauti kwenye mitandao ya kijamii baada ya Rais John Magufuli kupokea ripoti ya mchanga wa madini Ikulu, leo.

Katika akaunti yake ya Twitter, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameandika, “pongezi kwa kazi nzuri iliyofanywa na tume.” 

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe katika ukurasa wake wa Twitter ameandika, “utafiti unapingwa kwa utafiti. Kwa sasa Kamati ya Mruma Ndio rejea sahihi kwenye suala la mchanga na hivyo nakubali mapendekezo yaliyomo.”

Naye, Naibu Waziri Afya, Hamis Kigwangalla katika akaunti yake yaTwitter ameandika, “sishangai kumsikia Rais wetu akisema 'wasomi' tumeiangusha nchi. Kwa kila namna tunapaswa kujitazama sana.”

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ameandika, “nimemsikiliza mheshimiwa Rais na kuendelea kuielewa nia yake njema ya kuisaidia nchi yake. Tuko pamoja na ninakuunga mkono.”


Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye naye amempongeza Rais John Magufuli kwa kazi iliyofanywa na tume ya uchunguzi wa sakata la mchanga.

Nape anaungana na baadhi ya wabunge ambao pia wamempongeza Rais Magufuli kutokana na kazi aliyofanya kupitia tume hiyo.


Kupitia akaunti yake ya Twitter, Nape ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Machi mwaka huu, ameandika, “hili la mchanga...big up!” 

Baada ya kundolewa kwenye nafasi ya uwaziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo nafasi hiyo sasa inashikiliwa na Dk Harrison Mwakyembe ambaye alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria.
Nape, Tundu Lissu, na Zitto Kabwe wafunguka kuhusiana na ripoti ya mchanga Nape, Tundu Lissu, na Zitto Kabwe wafunguka kuhusiana na ripoti ya mchanga Reviewed by Zero Degree on 5/24/2017 03:40:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.