Loading...

Alichosema Mourinho kuhusiana na mpango wa kumsajili Cristiano Ronaldo


Meneja wa Manchester United amekana kuwa kuna mpango wa kumsaini Cristiano Ronaldo kutoka Real Madrid.

BBC iliripoti mwezi Juni kuwa Ronaldo alikasirishwa baada ya kushutumiwa kukwepa kulipa kodi na anataka kuondok Uhispania.

Kujiunga na Manchester United, klabu ambayo aliihama kwa kima cha pauni milioini 180 mwaka 2009 kilitajwa kama kile angeweza kuhamia.

Lakini baada ya kuulizwa kuhusu uwezekani huo, Mourinho alisema kuwa hilo haliwezi kufanyika kutokana na hali ngumu wa kiuhumi kuwezesha kandarasi kama hiyo.

"Ronaldo ni mchezaji muhimu sana kwa klabu yake. Mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kiuchumi. Hatujapa sababu yoyote ambayo itasababisha tufikirie kuwa Ronald anaweza kuondoka."

Maourinho aliongeza kuwa haamini kama mchezaji mwingine wa Real Madrid, Alvaro Morata anaweza kuhamia Manchester United.
Alichosema Mourinho kuhusiana na mpango wa kumsajili Cristiano Ronaldo Alichosema Mourinho kuhusiana na mpango wa kumsajili Cristiano Ronaldo Reviewed by Zero Degree on 7/16/2017 01:33:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.