Loading...

Dembele atua Barcelona na kuwa mchezaji wa pili aliyeghali zaidi katika historia ya soka


Barcelona Imekubali kandarasi ya kumsajili mshambuliaji wa Borrusia Dortmund Ousmane Dembele kwa kitita kinachotazamiwa kupanda hadi Yuro milioni 147 na kumfanya kuwa mchezaji wa pili aliyeghali katika historia ya soka.

Barca watalipa Yuro milioni 105 kwa mshambuliaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 20 ambaye amekubali kandarasi ya miaka mitano na atafanyiwa ukaguzi wa matibabu siku ya Jumatatu.

Mkataba huo umepitwa na ule wa Neymar wa uhamisho wa Pauni milioni 200 kwa klabu ya PSG.

Dembele hajaichezea Dortmund tangu mechi ya kombe la Supercup mnamo tarehe 5 mwezi Agosti.

Timu hiyo ya Ujerumani ilikataa ombi kutoka kwa Barcelona kumununua mchezaji huyo mnamo mwezi Agosti, wakati ambapo mchezaji huyo alikuwa amepigwa marufuku kwa kukosa mazoezi.

Dortmund imesema kuwa ilikataa ombi la Barcelona kwa kuwa halikuandamana na thamani ya mchezaji huyo pamoja na hali ya kichumi ya sasa.


Kujiunga kwa Dembele na timu hiyo sasa safu ya ushambulizi itakuwa MSD badala ha ilivokuwa MSN kabla Neymar hajaondoka.

Maana yale sasa itatambulika kama Lionel Messi, Luis Suarez na Dembele.
Dembele atua Barcelona na kuwa mchezaji wa pili aliyeghali zaidi katika historia ya soka Dembele atua Barcelona na kuwa mchezaji wa pili aliyeghali zaidi katika historia ya soka Reviewed by Zero Degree on 8/25/2017 08:50:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.