Loading...

Kilichomponza Tshishimbi Songea chaanikwa


LICHA ya kujulikana kuwa ni mmoja wa wachezaji wenye uwezo wa juu ingawa ana muda mfupi katika soka la Tanzania, kiungo wa Yanga, Papi Tshishimbi, juzi alipata wakati mgumu kucheza soka lake la pasi kutokana na mazingira aliyokutana nayo.

Tshishimbi ambaye katika mchezo huo alionekana kucheza soka la nguvu kama ilivyo kawaida yake, kila mara alipokuwa akigusa mpira ulikuwa ukipotea mguuni na wakati mwingine kila alipotoa pasi bado ilienda ndivyo sivyo, hiyo ikasababisha aanze kucheza soka la nguvu zaidi na kumfanya kuwa na wakati mgumu kupambana na viungo wa Majimaji.

Katika kipindi cha kwanza, Tshishimbi alipiga pasi tatu ambazo zote zilipotea njia na kwenda kwingine kutokana na mpira kudunda na kupoteza mwelekeo tofauti na aliokuwa akiutaka.

Katika kipindi hichohicho alipiga pasi mbili zilizoelekea langoni kwake ‘maboko’ wakati nia yake ilikuwa ni kupeleka kwenye lango la Majimaji.

Kwa bahati mbaya Tshishimbi mwenyewe hakupatikana kuzungumza juu ya mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa aliuzungumzia mchezo huo kwa kusema timu yake ilipoteza pasi nyingi kutokana na mazingira ya uwanja kutokuwa rafiki.
Kilichomponza Tshishimbi Songea chaanikwa Kilichomponza Tshishimbi Songea chaanikwa Reviewed by Zero Degree on 9/18/2017 04:02:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.