Loading...

Ombi la Neymar kwa Rais wa PSG juu ugomvi wake na Edison Cavani

Neymar (kushoto) anaripotiwa kuumbo uongozi wa PSG umuuze Edinson Cavani (kulia) ili kumaliza tofauti zao  
Neymar ameuomba uongozi wa Barcelona kumuuza mchezaji mwenzake, Edison Cavani.

Kwa mujibu wa taarifa ya chombo cha habari nchini Spain, mbrazili huyo ameweka hisia zake wazi kwa viongozi wa klabu hiyo.

Anaonelea kwamba mahusiano yake na Cavani ndani ya uwanja hayawezi kuwa mazuri tena kufuatia tukio la kugombani penati lilotokea siku ya jumapili PSG ilipoibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Lyon.

Chanzo hicho kinaripoti kwamba: "Neymar tayari amewasiliana na Nasser Al-Khelaifi kwamba uwepo wake yeye na Cavani hautowezekana na amemuomba amuuze raia huyo wa Uruguay."

Mmiliki huyo wa PSG sasa atatakiwa kufanya uamuzi kujaribu kumaliza tatizo hilo kati ya mchezaji ghali zaidi duniani (Neymar) na nyota wake aliyedumu kwa muda kidogo ndani ya klabu (Cavani).
Ombi la Neymar kwa Rais wa PSG juu ugomvi wake na Edison Cavani Ombi la Neymar kwa Rais wa PSG juu ugomvi wake na Edison Cavani Reviewed by Zero Degree on 9/19/2017 07:53:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.