Loading...

Yanga yalazimishwa sare ya bila kufungana


Mabingwa watetezi Ligi kuu Tanzania Bara, Yanga SC wameshindwa kufurukuta mbele ya wapinzani wao Mtibwa Sugar kwa kutoa sare ya bila ya kufungana katika mchezo wa Ligi Kuu uliyopigwa katika dimba la Uhuru Jijini Dar es Salaam jioni ya leo.


Mchezo huo ambao ulikuwa na mshambulizi ya piga ni kupige, Yanga walionekana kupata nafasi nyingi za kushambulia mlango wa wapinzani wao lakini kwa bahati mbaya juhudi zao ziligonga mwamba na kupelekea mpaka kipenga cha mwisho kupulizwa na mwamuzi wa mchezo huo wa mzunguko wa tano Ligi Kuu kutoka sare ya bila ya kufungana.

Kutokana na matokeo hayo, Yanga imefikisha alama tisa baada ya kucheza michezo mitano, sare tatu huku ikishinda mechi mbili, wakati Mtibwa Sugar ibafikisha pointi 11 baada ya sare hiyo ya pili, na kushinda mechi tatu.

Kwa upande mwingine, timu ya Ndanda imeibuka na ushindi kwa kuichapa Lipuli FC mabao 2-1, Mwadui akitoa sare ya kufungana 2-2 dhid ya Mbeya City, Mbao FC ikitoa sare ya bao 1-1 na Prisons huku Singida United nayo ikilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Azam FC.
Yanga yalazimishwa sare ya bila kufungana Yanga yalazimishwa sare ya bila kufungana Reviewed by Zero Degree on 9/30/2017 06:59:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.