Loading...

Nyumba za Lugumi zashindikana kuuzwa


Mnada wa nyumba ya pili za mfanyabiashara maarufu Said Lugumu, zilizopo maeneo ya Upanga jijini Dar es Salaam umeahirishwa Ijumaa hii.

Mnada huo ambao umekuwa ukisimamiwa na kampuni ya Yono, umeahirishwa kutokana na sababu za wateja ambao walitaka kununua nyumba hiyo kushindwa kufika bei ambayo ilitakiwa kuuzwa.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mnada ya Yono, Scolastica Kevela (kulia) akiwa eneo la mnada Mbweni leo
Wateja ambao walitakiwa kununua nyumba hiyo walikwamia kwenye bei ya shilingi milioni 650.

Wakati huo huo katika nyumba ya kwanza iliyopo katika eneo la Mbweni JKT ilishindwa kununuliwa kutokana na tatizo kama hilo baada ya wanunuzi wa mwisho kukwamia kwenye bei ya shilingi milioni 510.
Nyumba za Lugumi zashindikana kuuzwa Nyumba za Lugumi zashindikana kuuzwa Reviewed by Zero Degree on 11/24/2017 05:16:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.