Loading...

Alichosema Babu Seya baada ya kumuona Rais Magufuli

Familia ya Nguza baada ya kukutana na Rais Magufuli
MWANAMUZIKI nguli wa Dansi Nguza Vicking “Babu Seya” amesema ana furaha kubwa kuonana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kuomba kuonana nae kwa muda mrefu mbali na hilo wamemuombea.


Babu Seya ameyasema hayo alipofika Ikulu jijini Dar es salaam, Leo Januari 2, 2018 kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kwa msamaha wake aliotoa kwao dhadi ya kifungo cha maisha.

“Yaani sijui nisemeje, hapa nina furaha kubwa sana Moyoni mwangu, nilikuwa naomba sana tangu muda mrefu nikutane nae, nimeomba sana, hatimaye leo nimefanikiwa na nimemwambia namshukuru sana kwa kutusamehe na sasa nipo Tayari kuchapa kazi, Hapa Kazi Tu,” Nguza Viking (Babu Seya).

Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” aliongozana na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza.

Alichosema Babu Seya baada ya kumuona Rais Magufuli Alichosema Babu Seya baada ya kumuona Rais Magufuli Reviewed by Zero Degree on 1/02/2018 06:51:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.