Loading...

Nyota wa EPL anayetarajia kufanyiwa vipimo vya afya Chelsea


Kwa mujibu wa taarifa ya Paul Joyce, Ross Barkley anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya katika klabu ya Chelsea leo hii. Kiungo huyo wa Everton anatarajiwa kutua Stamford Bridge kwa pauni milioni 15.

ESPN pia wamethibitisha habari hiyo na kusema kwamba, Chelsea walikamilisha mazunguzo yao na nyota huyo tangu wiki iliyopita.

Chelsea walikuwa na nia ya kumsajili kwenye majira ya joto lakini mchezaji huyo alikataa. Barkley aliamua kwamba, haikuwa muda sahihi kwa yeye kujiunga na 'the Blues' kwa kipindi kile.

Tottenham pia walikuwa na nia ya kumsajili nyota huyo, lakini ESPN wanaripoti kwamba, klabu hiyo ilijitoa kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya kuwa klabu ya Chelsea imejitokeza kutaka kumsajili nyota huyo.


Everton wangeingiza kiasi cha pauni milioni 30 kama wangemuuza nyota huyo kwenye majira ya joto lakini ada hiyo imepungua kutokana na kwamba kiungo huyo amebakiza miezi sita kabla mkataba wake wa sasa haujamalizika.

Muingereza huyo anajiunga na Chelsea ikiwa ni sawa na ilivyokuwa kwa Frank Lampard na pia akiwa na rekodi sawa na za shujaa huyo wa Chelsea. Mashabiki wa 'The Blues' watakuwa na matumaini ya kuona walau 50% ya mafanikio ya Lampard katika klabu hiyo kutoka kwa Barkley.
Nyota wa EPL anayetarajia kufanyiwa vipimo vya afya Chelsea Nyota wa EPL anayetarajia kufanyiwa vipimo vya afya Chelsea Reviewed by Zero Degree on 1/05/2018 07:06:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.