Loading...

Kikosi kitakachoibeba Ufaransa kwenye Kombe la Dunia Urusi chatajwa


Mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial na Alexandre Lacazette wa Arsenal wameachwa nje ya kikosi cha Ufaransa kitakachoshiriki Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka huu.

Kiungo wa kati wa Marseille Dimitri Payet hayuko kwenye kikosi hicho cha Ufaransa.

Beki wa Manchester City Benjamin Mendy ni kati ya wachezaji wa Premier League walijuuishwa licha ya kurejea uwanjani mwezi Aprili baada ya karibu miezi ishirini kufuatia jeraha.

Kiungo wa kati wa Chelsea N'Golo Kante na mshambulizi Olivier Giroud, kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba na kipa wa Tottenham Hugo Lloris ni wachezaji wengine wanaosakata kabumbu England waliojumuishwa katika kikosi hicho cha wachezaji 23.

Kiungo wa kati wa Stoke Steven N'Zonzi pia naye amejumuishwa.

Mshambuliaji wa Bayern Munich Kingsley Coman na kiungo wa kati wa Paris St-Germain Adrien Rabiot pia nao wameachwa nje.

Ufaransa wako kundi la C pamoja na Australia, Peru na Denmark.

Kikosi kamili cha Ufaransa:

Walinda Lango: Hugo Lloris (Tottenham Hotspur), Steve Mandanda (Marseille), Alphonse Areola (Paris Saint-Germain)

Walinzi: Lucas Hernandez (Atletico Madrid), Presnel Kimpembe (Paris Saint-Germain), Benjamin Mendy (Manchester City), Benjamin Pavard (Stuttgart), Adil Rami (Marseille), Djibril Sidibe (Monaco), Samuel Umtiti (Barcelona), Raphael Varane (Real Madrid)

Viungo wa kati: N'Golo Kante (Chelsea), Blaise Matuidi (Juventus), Steven N'Zonzi (Sevilla), Paul Pogba (Manchester United), Corentin Tolisso (Bayern Munich)

Washambuliaji: Ousmane Dembele (Barcelona), Nabil Fekir (Lyon), Olivier Giroud (Chelsea), Antoine Griezmann (Atletico Madrid), Thomas Lemar (Monaco), Kylian Mbappe (Paris Saint-Germain), Florian Thauvin (Marseille)
Kikosi kitakachoibeba Ufaransa kwenye Kombe la Dunia Urusi chatajwa Kikosi kitakachoibeba Ufaransa kwenye Kombe la Dunia Urusi chatajwa Reviewed by Zero Degree on 5/19/2018 11:50:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.