Loading...

Trump aufuta mkutano wake na Kim Jong-un


Rais wa Marekani Donald Trump ameufuta mkutano wa kihistoria kati yake na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un uoliopangiwa kufanyika mwezi ujao.

Amesema uamuzi wake umetokana na "ghadhabu kuu na ukali wa wazi" uliokuwa kwenye taarifa ya karibuni ya Korea Kaskazini.

Bw Trump amesema haingekuwa vyema kuendelea na mkutano huo nchini Singapore Juni 12 kama ilivyokuwa imepangwa.


Kwenye barua kwa Bw Kim, amesema anasubiri sana kwa hamu kukutana naye "siku moja".

Trump amesema kuwa Marekani ilifahamishwa kuwa Korea Kaskazini ilikuwa imetuma maomba ya kufanyika kwa mkutano huo, lake kwa utawala wake hilo sio muhimu.

Rais huyo wa Marekani ameendelea kusema kwamba alikuwa na matarajio makubwa ya kukutana na kiongozi huyo wa korea kaskazini, lakini kutokana na hasira na uhasama wa wazi uliojitokeza katika taarifa ya hivi karibuni ya korea kaskazini, haoni ni muafaka kwa mkutano huo kuendelea kama ulivyopangwa.

Amesema kwa mujibu wa barua hiyo mkutano huo sasa hautafanyika.
Trump aufuta mkutano wake na Kim Jong-un Trump aufuta mkutano wake na Kim Jong-un Reviewed by Zero Degree on 5/24/2018 06:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.