Loading...

Azam yathibitisha kuachana na Himid Mao


Klabu ya Azam FC imethibitisha rasmi kuwa msimu ujao wa mwaka 2018/19 Ligi kuu ya Tanzania Bara haitakuwa na Nahodha wake na mchezaji wa muda mrefu, Himid Mao ‘Ninja’, ambaye ameomba ruhusa ya kwenda kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.

Hayo yamewekwa wazi na Afisa Habari wa Azam FC, Jaffery Iddy na kusema Himid ameomba kuondoka ndani ya Klabu hiyo ili kwenda nje kucheza soka la kulipwa.

"Sisi hatuna kipingamizi, Himid ni mchezaji wetu wa muda mrefu tokea akiwa mdogo kabisa ameshiriki mafanikio mengi ya timu, mara baada ya kuleta maombi hayo sisi tulimkubalia na tunamtakia kila la kheri huko aendako katika maisha yake mapya", amesema Maganga.

Msimu uliopita Himid Mao alikuwa anahusishwa kujiunga na klabu ya Yanga lakini swala hilo lilishindikana kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kutokana na mkataba na Azam FC.
Azam yathibitisha kuachana na Himid Mao Azam yathibitisha kuachana na Himid Mao Reviewed by Zero Degree on 6/01/2018 07:50:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.