Loading...

Chelsea yaanza kumnyemelea Alisson Becker

Alisson Becker
Matajiri wa Jijini London klabu ya Chelsea, wanajiandaa kuwania saini ya golikipa wa AS Roma Allison ili kuziba pengo la Thibout Coutors kama ataelekea Real Madrid.

Allisson mwenye uraia wa Brazil, alikuwa na msimu mzuri uliopita na kuingia katika rada za klabu nyingi ikiwemo Liverpool baada ya Karius kuonesha kiwango kibovu katika fainali ya UEFA Champions League.

Chelsea wanahitaji saini ya kipa huyo kwa udi na uvumba kufuatia kipa wao namba moja Thibaut Coutors kuwa katika mawindo ya Real Madrid kwa muda mrefu hivi sasa.

Allison anatajwa kuwa miongoni mwa walinda milango bora kwa sasa akichuana na David De Gea wa Manchester United, Ter stargen wa Barcelona na wengine wenye ubora sawa na hao.
Chelsea yaanza kumnyemelea Alisson Becker Chelsea yaanza kumnyemelea Alisson Becker Reviewed by Zero Degree on 6/01/2018 12:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.